Search This Blog

24 August 2012

HABARI MBALI MBALI

s Posts

A TIPSY NIGHT WITH CHRIS BROWN'S OFFICIAL DJ - DJ BABEY DREW

Posted by Global Publishers on August 24, 2012 at 11:58am 0 Comments
A TIPSY NIGHT WITH CHRIS BROWN'S OFFICIAL DJ - DJ BABEY DREW

JK AMWITA DIAMOND IKULU

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 10:07am 1 Comment
Stori: Sifael Paula
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amemuita ikulu mwanamuziki anayefanya vizuri kwa sasa kwenye Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kumpa jukumu maalum, Ijumaa linairusha hewani.
Kwa mujibu wa Diamond, juzikati ‘prezidenti’ alimwita ikulu Magogoni, Dar es Salaam na kumpa shavu la kwenda kufanya shoo kwenye mkutano maalum utakaofanyika Washington DC nchini Marekani hivi karibuni.
“Yaa, rais aliniita akaniambia kuna shoo natakiwa kwenda kufanya Marekani.

“Kwa mara ya kwanza nitasafiri nje ya nchi na madensa wangu wanne na msemaji mmoja. Sasa hivi hawataki kutembea na kupanda magari wasije wakakosa hiyo safari,” alisema Diamond na kuongeza kuwa baada ya kuumwa, mawazo aliyaweka kwenye mchongo huo…

NDOA YA HUSNA MAULID NAYO CHALI

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 10:00am 0 Comments

Stori: Shakoor Jongo na Musa Mateja

WASWAHILI wanasema, ngoma ikivuma sana mwishowe hupasuka! Usemi huo ulikamilika juzikati kufuatia taarifa kwamba ndoa ya mshiriki wa Shindano la Miss Tanzania 2011, Husna Maulid iliyofungwa Juni mwaka huu imevunjika.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, ndoa hiyo imeingia kirusi kufuatia mazingira ya kutokuelewana kati ya Husna, ndugu wa mume pamoja na mumewe aliyefahamika kwa jina la Aboubakar ‘Abuu’.
“Nilisema mimi ndoa za mastaa ni vigumu sana kudumu, ya Husna nayo chali, kama vipi fuatilieni,” kilitutonya chanzo hicho…

ALIYEFUNGASHIA: HALIMA MDIWA

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 11:18am 0 Comments
A.K. A: Aunty Suzy

UMRI: 25

KABILA: Mpare

KAZI YAKE: Uigizaji

MAKAZI: Kinondoni, Dar.
AMEPATAJE MAKALIO HAYO?

“Yaani ukiniuliza nimelipataje wala sina jibu kwa kuwa nimelishangaa linakuja tu tangu nikiwa mdogo. Mbaya zaidi mama yangu yuko kawaida tu, siyo mnene.”
USUMBUFU ANAOKUTANA NAO

“Umbile langu linanifanya nawakimbie wanaume, kila nikipita mara huyu kanikonyeza, mara huyu kananiita, yaani ni usumbufu mtindo mmoja.”
ANATAMANI KUPUNGUA

“Mimi natamani sana kupungua ndiyo maana natumia…

MAGARI YA MASTAA…KAMA ULAYA, KAMA BONGO

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 10:07am 0 Comments
Na John Joseph
MAISHA ya mastaa wa Ulaya na kwingineko ni kuonyesha ufahari wa mali wanazomiliki, utamaduni wa aina hiyo ni mgeni nchini lakini kwa sasa unashika kasi kwa kuendelezwa na watu maarufu. Pichani juu ni magari halisi na mifano ya yale ambayo yanamilikiwa na mastaa katika tasnia ya burudani na michezo Tanzania.

IJUMAA SEXIEST GIRL WOLPER, AGNES WAKALIA KUTI KAVU

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 11:00am 2 Comments
MPAMBANO ni mkali na sasa washiriki wawili, Jack Wolper na Agnes Gerald mmoja wao yuko kwenye hatihati ya kutolewa kwenye shindano hili baada ya kupigiwa kura nyingi za kufungana.

Mratibu wa shindano hili, Imelda Mtema alisema: “Hakika mtifuano ni mkali sana, kura zilizopigwa wiki hii ni nyingi lakini Agnes na Wolper wamegongana hivyo hakuna atayetoka ila wiki ijayo mmoja kati yao atachapa lapa.”

Hata hivyo wasomaji wametakiwa kuendelea kumpigia kura mshiriki mmoja anayestahili kutoka kwa kuandika jina lake kisha kulituma kwenda namba 0786-799120. Nani atatoka wiki ijayo? Tusubiri…

SHEHE SHARIFU AZAWADIWA MKE

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 10:01am 1 Comment


Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
SHEHE Sharifu Mikidadi Matongo ambaye alijizolea umaarufu tangu alipokuwa mdogo, ameanika wake zake wawili huku akieleza kuwa, mmoja alipewa zawadi.
Akipiga stori na Ijumaa nyumbani kwake Magomeni Mwembechai jijini Dar, Shehe Sharifu alisema alifunga ndoa na mke wake wa kwanza mwaka 2006 baada ya kuzawadiwa na Ikulu ya Komoro alipoomba dua na kufanikisha kupatikana kwa maiti zilizokuwa zimepotea baada ya ajali ya meli.
“Mke wangu wa kwanza anaitwa Mwanasharifu Hussein, nilimpata kama zawadi nilipokuwa nimetembelea Komoro ambako niliomba dua na kuzawadiwa na rais wa nchi hiyo,” alisema.
Akaongeza kuwa, pamoja na kuzawadiwa mke huyo, alipomuona tu alimpenda sana na alikuwa kwenye mipango ya ndoa, hivyo wakakubaliana na kuoana.
Alidai kuwa, baadaye alioa mke wa pili hapa nchini aitwaye Shamsa Hemedy na sasa anaishi nao wote wawili kwa furaha. Aidha, amekanusha madai ya kwamba…

HOYCE TEMU MFANO WA KUIGWA

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 10:00am 1 Comment
Na Imelda Mtema

JAPOKUWA imetimia miaka 14 tangu alipotwaa taji la Miss Tanzania mwaka 1999, bado Hoyce Temu anaendelea kuaminika kuwa ndiye mrembo wa mashindano hayo aliyeitumikia jamii zaidi kuliko wengine wote.

Hoyce ambaye kwa sasa anaendesha kipindi cha Mimi Na Tanzania katika Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, amekuwa akijihusisha na jamii ya watu wa chini kwa kuwasaidia kupitia kipindi chake…

KUACHWA KUPO TU, MUDA UKIFIKA HUNA SABABU YA KUUMIA!

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 9:55am 0 Comments
WIKI hii mpenzi msomaji wangu nataka kuzungumzia hii ishu ya wapenzi kutosana. Katika ulimwengu wa sasa tumekuwa tukishuhudia wapenzi waliotokea kupendana sana wakiachana tena wakati mwingine katika mazingira yasiofaa.
Hilo si la kushangaa kwani limekuwepo tangu enzi za mababu zetu, walipendana lakini pia wapo waliokuwa wakiachana kwa mateke na mangumi.
Haya hivyo, kuachwa ukusikie hivihivi kwa wenzako, inauma sana pale unapomkosa mtu ambaye huenda ulishaamini atakuwa wako wa maisha. Maumivu ya kuachwa ndiyo yanayowafanya baadhi ya watu kufikia hatua ya kuchanganyikiwa na wengine kunywa sumu.
Ndiyo maana wataalam wa masuala ya mapenzi wanasema, usiombe ukaachwa. Bora ukishaona dalili ya kuachwa ukawahi kuacha wewe ili angalau kujipunguzia…

TIKO AAPA KUMZALIA MUME WA MTU MTOTO MMOJA TU

Posted by GLOBAL on August 24, 2012 at 9:59am 1 Comment

Stori: Gladness Mallya
MSANII wa filamu za Kibongo ambaye anatishia kuwafunika wakongwe, Tiko Hassan ameonesha kulikomalia penzi la mume wa mtu na kusema kwamba, yuko tayari kuzaa naye angalau mtoto mmoja.
Akichezesha taya na paparazi wetu, hivi karibuni,Tiko alisema anaumia kuingilia penzi la mwanamke mwenzake lakini kwa kuwa mwanaume huyo (hakupenda kulianika jina lake) anaonesha kumpenda yeye zaidi, bora aambulie hata damu yake tu.
Alisema, katika maisha yake amepita kwa wanaume kadhaa lakini kwa huyo anaona bora atulie na kuyaacha maisha yaendelee.
“Huyu ndiye mwanaume niliyekuwa nikimhitaji, ananijali na tangu tumekuwa wapenzi hatujawahi kuwa na ugomvi mkubwa ila wa kawaida tu, hivyo niko tayari kumzalia mtoto mmoja tu,” alisema Tiko.